Chapati za Maziwa na Mayai.


chefzey

Mahitaji

  1. Unga WA Ngano vikombe  8.
  2. Maji au maziwa  au mchanganyiko  wa maji na maziwa vikombe 2 na nusu.
  3. Siagi au margarine (blue band  au prestige)  vijiko 4  vya kukandia .
  4. Margarine au siagi  ya kukunjia  robo kikombe .
  5. Vanilla  kijiko 1 cha chai .
  6. Hiriki ya unga  kijiko
  7. kimoja cha chai .
  8. Mafuta ya kukunjia  na kuchomea  nusu kikombe .
  9. Unga WA kusukumia  kikombe kimoja .
  10. Chumvi  vijiko 3 vya chai .
  11. Sukari  kijiko kimoja  na nusu cha chakula .
  12. Mayai 3.

Jinsi ya kupika .

  • Chukua unga wako chekecha  kisha weka ndani ya chombo cha kukandia.
  • Chukua mayai  kisha yapige kwa pembeni.
  • Chukua siagi yote kisha yeyusha.  
  • Weka tobo katikati  kisha weka vanilla  ,hiriki, Sukari  ,Chumvi  na mayai yako kisha weka na siagi. 
  • Kisha  changanya  kwa Mikono yote 2 huku una sugua  sugua.
  •   kisha vikishachanganyika anza kuweka maziwa au maji au mchanganyiko wa maji na maziwa.
  •  kisha kanda kidogo  Chukua  mafuta  ya kupikia kijiko  1 cha chai pakaza  kwa juu ili donge  lako lisiwe kavu na kuweka Ugumu  kwa juu.
  •  kisha funika  Kwa saa moja. 
  • Baada ya saa moja funua  kanda  tena Kata madonge yako  10 mpaka 13. 
  • Kisha funika Kama dakika  10. 
  • Anza kufanya  tabaka  ( unasukuma  chapati  yako kisha unapaka  margarine  au mchanganyiko  wa margarine  na mafuta kisha una nyunyiza unga  unatengeneza  tabaka Fanya hivyo  kwa zote kisha acha kama dakika 15).
  • Bandika chuma cha kuchomea  jikoni kikipata moto sukuma chapati  yako  weka jikoni acha iive geuza upande  wa pili acha dakika 1.
  • Anza kuweka mafuta  pia hadi chapati  zako ziive kote kote.

Comments